Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki katika ujenzi wa bwawa la maji katika kata ya kijiji cha Marika jimbo la Lulindi wakati akiwa katika ziara jimboni humo akikagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM ya Mwaka 2010 inayotekelezwa na serikali na kuhimiza uhai wa chama katika jimbo hilo lililop0 wilaya ya Masasi mkoani Mtwara, Katika ziara hiyo ya mikoa ya Lindi na Mtwara Kinana anaongozana na Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikasi, Siasa na Uenezi. Kesho Kinana anaendelea na ziara katika wilaya ya Newala.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-LULINDI -MASASI)
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi mara baada ya kukagua ujenzi wa bwawa la maji katika kijiji cha Marika.
Mtambo wa kuchimbia mifereji ukiendelea na kazi ya kutengeneza tuta la bwawa hilo katika kijiji cha Marika.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akionyesha kadi zilizorejeshwa na wapinzani na kujiunga na CCM katika kata ya Chungutwa jimbo la Lulindi kushoto ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mtwara ndugu Mohamed Sinani.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na mbunge wa jimbo la Lulindi Mh.Jerome Bwanausi
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki ujenzi wa tanki la maji kwa kupiga ripu wakati alipotembelea na kukagua ujenzi wa mradi wa maji wa Chiungutwa jimboni Lulindi.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikagua vikundi vya ngoma alipowasili katika kata ya Chiungutwa.
Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikasi, Siasa na Uenezi akimtunza kiongozi wa kwaya ya Chiungutwa wakati ilipokuwa ikitumbuiza.
Afisa CCM makao makuu Lumumba Bi. Gift Msuya akikitunza kikundi cha kwaya cha Chiungutwa wakati kilipokuwa kikitumbuiza katika mkutano huo.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwaongoza wanachama wapya kula kiapo cha utii kwa chama kulia ni Katibu wa CCM mkoa wa Mtwara Ndugu Shaibu Akwilombe.





No comments:
Post a Comment