Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam mara baada ya kumalizika kwa kikao cha Kamati Kuu ambapo alisema
Kamati Kuu ya CCM imepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za
kusikitisha za kifo cha Mjumbe wa halmashauri kuu wa miaka mingi, msanii wa
chama cha mapinduzi, kada mzoefu Kapteni John Komba,
Kwa maneno ya Mwenyekiti wa CCM kifo cha Komba ni pengo lisilozibika, Chama
Cha Mapinduzi kimepata pigo kubwa ,
Komba atabaki kwenye historia iliyotukuka kwenye Chama Cha
Mapinduzi.
Pia Kamati Kuu imewasimamisha Profesa Anna Tibaijuka ambaye ni mjumbe wa Kamati Kuu,Andrew Chenge ambaye ni mjumbe wa Halmashauri Kuu pamoja na Wiliam Ngeleja Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kuhudhuria vikao vya maamuzi vya chama kwa kipindi ambacho kamati hii ndogo ya
maadili wakiendelea na kazi yao ya kupitia baadhi ya nyaraka mbali mbali
zinazohusiana na suala hili.
Akizungumzia kuhusu adhabu walizopewa wale wanachama sita waliojitokeza na kuanza shughuli za kampeni za kuwania nafasi ya kuchaguliwa na chama kugombea urais alisema kamati ndogo ya maadili inaendelea na uchunguzi wake.

No comments:
Post a Comment