Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kazi ya kuchimba mtaro pamoja na viongozi wa mkoa wa Dodoma kwa ajili ya kufukia mabomba katika mradi wa maji wa Kata ya Mundemu kijiji cha Nguji katika wilaya ya Bahi wakati alipotembelea mradi huo na kukagua shughuli za ujenzi wa tanki la maji na usambazaji wa mfumo wa mabomba akiwa katika ziara yake ya kikazi mkoani Dodoma, Kinana yuko Katika ziara ya mikoa ya Dodoma, Arusha na Kilimanjaro akikagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 akiongozana na msemaji wa chama hicho Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Bw. Nape Nnauye pamoja na viongozi mbalimbali wa chama na serikali katika mkoa wa Domoma.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-BAHI-DODOMA)
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi wa kijiji cha Nguji kata ya Mundemu mara baada ya kukagua mradi huo na kushiriki katika shughuli za ujenzi.
Kutoka kulia ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dodoma Mh. Adam Kimbisa, Mh. Badwel Mbunge wa jimbo la Bahi na Luteni Mstaafu Chiku Galawa Mkuu wa mkoa wa Dodoma wakimsikiliza Ndugu Abdulrahman Kinana hayupo pichani wakati alipokuwa akizungumza na wananchi katika kijiji cha Nguji.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikagua mradi wa umeme wa jua ambao ni maalum kwa ajili ya kuendesha kisima cha maji ya kumwagilia mashamba ya zabibu.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na wananchi mbalimbali wakati alipotembelea miradi mbalimbali katika wilaya ya Bahi ili kujioneautekelezaji wake.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiongozana na Mkuu wa mkoa wa Dodoma Luteni Mstaafu Chiku Galawa huku wakiwa wameshika majembe tayari kwa kushiriki katika shughuli ya kusafisha shamba la Zabibu.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na ujumbe wake wakiendelea na shughuli za kusafisha shamba kwa ajili ya upandaji wa miche ya mizabibu.
Moja ya nyumba za walimu zinazojengwa katika kijiji cha Kongogo kata ya Babayu ambayo katibu mkuu aliikagua na kushiriki katika ujenzi wake.
Mbunge wa jimbo la Bahi Mh. Badwel akizungumza na wananchi huku Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimsikiliza katika kijiji cha Kongogo.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akivishwa mgorole kama ishara ya kupewa heshima ya wazee wa kijiji cha Chonde.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipungiana mkono na wananchi mara baada ya kupewa heshima ya wazee wa kijiji cha Chonde kwa kumvisha mgorole.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizindua mradi wa matrekta katika kijiji cha Chonde ambapo vikundi 12 vinamiliki matrekta 19 yanayofanya kazi ya kilimo katika mashamba ya wanavikundi na wananchi kwa ujumla. 
Nape Nnauye naye akiendesha moja ya matrekta mara baada ya kuzinduliwa rasmi na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana katika kijiji cha Chonde.
Wananchi wakinyoosha mikono yao juu kuashiria kukubali hotuba ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana wakati alipokuwa akizungumza nao katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Chonde.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi wa kijiji cha Chonde wilayani Bahi wakati alipofanya ziara yake katika wilaya hiyo.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipokelewa na mamia ya wananchi katika kijiji cha Chonde ambapo pia ameshiriki katika shughuli ya ujenzi wa zahanati ya kijiji hicho.
Nape Nnauye akiwasili katika eneo la mkutano katika kijiji cha Chonde.
No comments:
Post a Comment