Saturday, 23 May 2015

MWENYEKITI WA CCM TAIFA MH. JAKAYA KIKWETE ATEMA CHECHE KWA WAJUMBE WA NEC MJINI DODOMA

indexMWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi(CCM), Rais Jakaya Kikwete 

amesema  uchaguzi mkuu mwaka huu, lazima chama hicho 

kihakikishe kinateua wagombea wanaozika na kukubalika kwa wananchi 

kwa ngazi zote kuanzia udiwani, ubunge na urais huku akitaka chama hicho 

kusoma alama za nyakati.

Rais Kikwete amesema  hayo leo mjini  wakati anafungua kikao cha 

Halmashauri Kuu(NEC) ya chama hicho kiliachoanza kikao chake cha siku 

mbili leo jioni ambapo ametumia nafasi hiyo kuzungumzia mchakato wa 

uchaguzi mkuu.

Amesema kuwa  wajumbe wa halmashauri kuu wahakikishe 

wanachagua mgombea anayekubalika kwa wananchi huku  akiendelea kufafanua kuwa 

wana CCM wapo milioni sita lakini watanzania wanaopiga kura ni milioni 

23.

“Msipochagua watu wanaokubalika na kuuza kwenye uchaguzi mkuu 

mtajikuta  mnashindwa hata kuwa chama cha kwanza cha upinzani 

kutokana na matokeo mabaya mtakayoyapata,”alisema Rais Kikwete.

amesema CCM itambue kuwa kama wao watapitisha jina la mgombea 

kwasababu ya kuogopana , basi wananchi hawatawaogopa na watachagua 

mtu kulingana na mahitaji yao.Hivyo CCM mkahakikishe anayechaguliwa 

basi anakubalika kwa wananchi.

“Lazima tuwe na wagombea wataakaokubalika kwetu na jamii ya 

kitanzania.Tukipeleka mtu ambaye hakubaliki kwa wananchi itakula 

kwetu,lazima tutambue alama za nyakati,”alisema.

Rais Kikwete alisema kama CCM wanaogopana , watambue wananchi 

hawawaogopi ila lazima pia ifahamike chama kwanza ,mtu baadae.

“Tunajukumu la kutafua wagombea watakaotuletea heshima , pia maslahi 

ya chama ni makubwa kuliko ya mtu mmoja mmoja.Hivyo tufanye  mambo 

kwa misingi tuliyojiwekea,”alisema Kikwete.
Amewakumbusha wana CCM 

usemi wa Mwalimu Julius Nyerere kwamba Rais anaweza kutoka chama 

chochote lakini Rais bora atatoka CCM.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa CCM Abdulrhaman Kinana alisema 

jumla wajumbe wote ni 574 lakini waliokuwepo kwenye kikao cha jana 

ilikuwa ni 342 sawa na asilimia 92.

No comments:

Post a Comment