………………………………
Rais wa Msumbiji Mhe. Filipe Nyusi ameahidi kueleleza ushirikiano wa pamoja katika kukuza na kuendeleza Chuo cha Diplomasia kilichopo Kurasini Jijini Dar es Salaam ili kuweze kuwa chuo chenye kiwango cha juu cha Kimataifa.
Kauli hiyo ilitolewa leo na Rais Nyusi wakati alipotembelea chuo hicho, ambapo alisema katika mazungumzo yake na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe .Dkt . Jakaya Mrisho Kikwete wamezungumzia jinsi ya kukiimarisha ili kiweze kuwa kumbukumbu ya wapigania uhuru si kwa nchi hizo bali hata kwa nchi za Kusini wa Afrika.
“Mimi na Rais Kikwete katika mazunguzo yetu ya jana , tumezungumzia jinsi ya kuendeleza kituo hiki .” alisema Rais Nyusi.
Aidha Rais Nyusi aliahidi kutoa nafasi ya kubadilishana uzoefu katika mafunzo kupitia ushirikiano huo, ambapo wanafunzi wa chuo hicho na wakufunzi watakuwa wanakwenda Msumbiji kwenye .
Aidha Rais Nyusi aliwataka wanafunzi wa chuo hicho, kujiandaa kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika serikalini na sekta binafsi wakiwa wanadiplomasia badala ya kutegemea kuwa mabalozi.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi wa Chuo hicho, Balozi Mwanahidi Majaar alisema wanampango wa kukiboresha chuo hicho ili kiweze kuwa chuo bora cha kimataifa katika nchi zilizo Kusini mwa Afrika.

No comments:
Post a Comment