Monday, 16 March 2015

CHADEMA KARATU YAVITENGA VIJIJI VINAVYOONGOZWA NA CCM KATIKA HUDUMA ZA MAENDELEO

Mfano mradi wa Kituo cha afya cha Baray Mbuga Nyekundu ambapo serikali kuu ilitenga na kupeleka fedha kiasi cha shilingi milioni 60 katika halmashauri hiyo kwa ajili ya ujenzi wa majengo ya kituo hicho, lakini fedha hizo zimeondolewa katika mradi huo na madiwani hao na hazijulikani zimefanya kazi gani huku wananchi wakitaabika kwa kutopata huduma nzuri za afya kijijini hapo.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-KARATU-ARUSHA)2Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kufukua mchanga kwenye mfereji unaopitisha maji kwa ajili ya kumwagilia mashamba ya vitunguu katika kijiji cha Mang’ola Barazani wilayani Karatu.3Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kupanda vitunguu pamoja na wananchi katika mashamba hayo.4Baadhi ya wananchi wakiwa wamekaa juu ya mti wakati walipokuwa wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana hayupo pichani alipozungumza nao kwenye mkutano wa hadhara kijijini Mang’ola.5Baadhi ya wananchi wakiwa wamekaa juu ya mti wakati walipokuwa wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana hayupo pichani alipozungumza nao kwenye mkutano wa hadhara kijijini Mang’ola.7Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi katika kjiji cha Mang’ola.9Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kumwaga zege katika ujenzi wa ofisi ya kijiji cha Rhotia wilayani Karatu.10Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiweka jiwe la msingi katika ukumbi wa kitegauchumi cha kijiji cha Kilimatembo mjini Karatu.11Mbunge wa viti maalum Kupitia vijana CCM mkoa wa Arusha Catherine Magige akiwasalimia maelfu ya wananchi waliojitokeza katika mkutano wa hadhara mjini Karatu. 12Umati wa wananchi wakifuatilia mkutano huo.14Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Omar Kwang akisalimia wananchi.15Mkuu wa mkoa wa Arusha Mh. Felix Ntibenda akiwasalimia wananchi.16Nape Nnauye akiwahutubia wananchi  katika mkutano wa hadhara uliofanyika leo mjini Karatu.17Nape Nnauye akisisitiza jambo katika mkutano huo18Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi na kujibu hoja mbalimbali ambapo aliwaambia maswali mengi yanaelekea kwa mbunge wa jimbo hilo, madiwani na mwenyekiti wa halmashauri kwa kuwa ndiyo wenye kusimamia miradi na kuwapa taarifa wananchi, Lakini viongozi hao wamekuwa wakifanya mambo wanavyotaka na kuacha wananchi wakipata taabu.

No comments:

Post a Comment